Yoe. 1:16-20 Swahili Union Version (SUV)

16. Je! Chakula hakikukatiliwa mbali mbele ya macho yetu? Naam, furaha na kicheko mbali na nyumba ya Mungu wetu?

17. Mbegu zinaoza chini ya udongo wake; ghala zimeachwa ukiwa; mabanda yamevunjika; kwa maana nafaka imekauka.

18. Jinsi wanyama wanavyougua! Makundi ya ng’ombe yamefadhaika, kwa sababu hawana malisho; naam, makundi ya kondoo yamepata mateso.

19. Ee BWANA, nakulilia wewe;Kwa maana moto umeyala malisho ya nyikani,Na miali ya moto imeteketeza miti yote ya mashamba.

20. Naam, wanyama wa mashamba wanakutwetea wewe;Kwa maana vijito vya maji vimekauka,Na moto umeyateketeza malisho ya nyikani.

Yoe. 1