Yn. 9:32-40 Swahili Union Version (SUV)

32. Tokea hapo haijasikiwa ya kuwa mtu ameyafumbua macho ya kipofu, ambaye alizaliwa hali hiyo.

33. Kama huyo asingalitoka kwa Mungu, asingeweza kutenda neno lo lote.

34. Wakajibu, wakamwambia, Ama! Wewe ulizaliwa katika dhambi tupu, nawe unatufundisha sisi? Wakamtoa nje.

35. Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu?

36. Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini?

37. Yesu akamwambia, Umemwona, naye anayesema nawe ndiye.

38. Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia.

39. Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu.

40. Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu?

Yn. 9