Yn. 7:13-15 Swahili Union Version (SUV)

13. Walakini hakuna mtu aliyemtaja waziwazi, kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.

14. Hata ikawa katikati ya sikukuu Yesu alikwea kuingia hekaluni, akafundisha.

15. Wayahudi wakastaajabu wakisema, Amepataje huyu kujua elimu, ambaye hakusoma?

Yn. 7