45. Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na Mungu. Basi kila aliyesikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu.
46. Si kwamba mtu amemwona Baba, ila yeye atokaye kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47. Amin, amin, nawaambia, Yeye aaminiye yuna uzima wa milele.
48. Mimi ndimi chakula cha uzima.
49. Baba zenu waliila mana jangwani; wakafa.
50. Hiki ni chakula kishukacho kutoka mbinguni, kwamba mtu akile wala asife.