Yn. 6:27-31 Swahili Union Version (SUV)

27. Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa muhuri na Baba, yaani, Mungu.

28. Basi wakamwambia, Tufanyeje ili tupate kuzitenda kazi za Mungu?

29. Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa na yeye.

30. Wakamwambia, Unafanya ishara gani basi, ili tuione tukakuamini? Unatenda kazi gani?

31. Baba zetu waliila mana jangwani kama vile ilivyoandikwa, Aliwapa chakula cha mbinguni ili wale.

Yn. 6