Yn. 20:4-7 Swahili Union Version (SUV)

4. Wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi mwingine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza kufika kaburini.

5. Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.

6. Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,

7. na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.

Yn. 20