Yn. 2:6-9 Swahili Union Version (SUV)

6. Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.

7. Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.

8. Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.

9. Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,

Yn. 2