1. Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
2. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3. Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
4. Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
5. Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.
6. Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.