Yn. 19:15-17 Swahili Union Version (SUV)

15. Basi wale wakapiga kelele, Mwondoshe! Mwondoshe! Msulibishe! Pilato akawaambia, Je! Nimsulibishe mfalme wenu! Wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.

16. Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe; nao wakampokea Yesu.

17. Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha.

Yn. 19