Yn. 16:5-9 Swahili Union Version (SUV)

5. Lakini sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi?

6. Ila kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu.

7. Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu.

8. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.

9. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;

Yn. 16