Yn. 16:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa.

2. Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada.

3. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.

4. Lakini nimewaambia hayo, ili makusudi saa ile itakapokuja myakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia.Sikuwaambia hayo tangu mwanzo, kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi.

5. Lakini sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi?

Yn. 16