Yn. 1:36-38 Swahili Union Version (SUV)

36. Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!

37. Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

38. Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?

Yn. 1