Yn. 1:14-16 Swahili Union Version (SUV)

14. Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.

15. Yohana alimshuhudia, akapaza sauti yake akasema, Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Ajaye nyuma yangu amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.

16. Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.

Yn. 1