Yn. 1:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

2. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

4. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.

5. Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.

Yn. 1