Yer. 49:9-17 Swahili Union Version (SUV)

9. Je! Kama wachuma zabibu wangekujia, wasingeacha zabibu ziokotwe? Kama wangekujia wevi usiku, wasingeharibu hata watakapopata vya kutosha?

10. Lakini nimemwacha Esau hana kitu, nimepafunua mahali pake pa siri, wala hataweza kujificha; kizazi chake kimeangamizwa, na ndugu zake, na jirani zake, naye mwenyewe hayuko.

11. Waache watoto wako wasio na baba, mimi nitawahifadhi hai, na wajane wako na wanitumaini mimi.

12. Maana BWANA asema hivi, Tazama, wale wasioandikiwa kunywea kikombe, watakinywea, ni hakika; na wewe je! U mtu ambaye hataadhibiwa kabisa? Hukosi utaadhibiwa, naam, kunywa utakunywa.

13. Kwa maana nimeapa kwa nafsi yangu, asema BWANA, kwamba Bozra utakuwa ajabu, na aibu, na ukiwa, na laana; na miji yake yote itakuwa ukiwa wa daima.

14. Nimepata habari kwa BWANA,Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa,Akisema, Jikusanyeni, mkaujie,Mkainuke kwenda vitani.

15. Maana nimekufanya mdogo kati ya mataifa,Na kudharauliwa katika watu.

16. Katika habari za kuogofya kwako,Kiburi cha moyo wako kimekudanganya,Wewe ukaaye katika pango za majabali,Ushikaye kilele cha milima;Ujapofanya kioto chako juu sana kama tai,Nitakushusha kutoka huko; asema BWANA.

17. Na Edomu atakuwa ajabu; kila mtu apitaye atashangaa, na kuzomea, kwa sababu ya mapigo yake yote.

Yer. 49