15. Maana nimekufanya mdogo kati ya mataifa,Na kudharauliwa katika watu.
16. Katika habari za kuogofya kwako,Kiburi cha moyo wako kimekudanganya,Wewe ukaaye katika pango za majabali,Ushikaye kilele cha milima;Ujapofanya kioto chako juu sana kama tai,Nitakushusha kutoka huko; asema BWANA.
17. Na Edomu atakuwa ajabu; kila mtu apitaye atashangaa, na kuzomea, kwa sababu ya mapigo yake yote.
18. Kama vile vilivyotokea wakati wa kuangushwa Sodoma na Gomora, na miji iliyokuwa karibu nayo, asema BWANA; hapana mtu atakayekaa huko, wala hapana mwanadamu atakayekaa huko kama mgeni akaavyo.
19. Angalia, atapanda kama simba toka kiburi cha Yordani juu ya malisho yasiyonyauka; lakini nitamkimbiza ghafula ayaache; na yeye aliye mteule nitamweka juu yake; maana ni nani aliye kama mimi? Tena ni nani atakayeniandikia muda? Tena ni mchungaji yupi atakayesimama mbele zangu?
20. Basi, lisikieni shauri la BWANA;Alilolifanya juu ya Edomu;Na makusudi yake aliyoyakusudiaJuu yao wakaao Temani;Hakika watawaburura, naam, wadogo wa kundi;Hakika malisho yao yatafadhaika kwa ajili yao.
21. Nchi yatetemeka kwa sauti ya kuanguka kwao;Kuna kilio, sauti yake yasikiwa katika Bahari ya Shamu.
22. Tazama, atapanda na kuruka kama tai, na kutandaza mabawa yake juu ya Bozra; na mioyo ya mashujaa wa Edomu siku hiyo itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wake.