Yer. 48:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Habari za Moabu. BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Ole wake Nebo! Kwa maana umeharibika; Kiriathaimu umeaibishwa, umetwaliwa; Misgabu umeaibishwa, nao umebomolewa.

2. Sifa za Moabu haziko tena; katika Heshboni wameazimia mabaya juu yake, Haya! Njoni, na tumkatilie mbali asiwe taifa. Wewe nawe, Ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.

3. Sauti ya kilio toka Horonaimu,Ya kutekwa na uharibifu mkuu.

4. Moabu umeharibika;Wadogo wake wamewasikiza watu kilio.

5. Kwa maana watu wapandapo huko LuhithiWatapanda wasiache kulia;Nao watu watelemkapo huko HoronaimuWameisikia huzuni ya kilio cha uharibifu.

6. Haya! Kimbieni! Jiokoeni nafsi zenu!Mkawe kama mtu aliye mkiwa.

7. Maana, kwa kuwa umeyatumainia matendo yako, na hazina zako, wewe nawe utatwaliwa; na Kemoshi atatoka aende katika uhamisho, makuhani wake na wakuu wake pamoja.

Yer. 48