Yer. 48:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Habari za Moabu. BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Ole wake Nebo! Kwa maana umeharibika; Kiriathaimu umeaibishwa, umetwaliwa; Misgabu umeaibishwa, nao umebomolewa.

2. Sifa za Moabu haziko tena; katika Heshboni wameazimia mabaya juu yake, Haya! Njoni, na tumkatilie mbali asiwe taifa. Wewe nawe, Ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.

3. Sauti ya kilio toka Horonaimu,Ya kutekwa na uharibifu mkuu.

4. Moabu umeharibika;Wadogo wake wamewasikiza watu kilio.

Yer. 48