Yer. 33:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Tena, neno la BWANA likamjia Yeremia mara ya pili, hapo alipokuwa akali amefungwa katika uwanda wa walinzi, kusema,

2. BWANA alitendaye jambo hili, BWANA aliumbaye ili alithibitishe; BWANA ndilo jina lake; asema hivi,

3. Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.

4. Maana BWANA, Mungu wa Israeli asema hivi, katika habari za nyumba za mji huu, na katika habari za nyumba za wafalme wa Yuda, zilizobomolewa ili kuyapinga maboma na upanga;

Yer. 33