Yer. 30:22-24 Swahili Union Version (SUV)

22. Nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.

23. Tazama, tufani ya BWANA, yaani, ghadhabu yake, imetokea tufani ya kudumu; itawaangukia waovu vichwani.

24. Hasira kali ya BWANA haitarudi, hata atakapokwisha kutenda, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtayafahamu haya.

Yer. 30