1. Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa BWANA, kusema,
2. BWANA Mungu wa Israeli, asema hivi, ya kwamba, Uyaandike kitabuni maneno hayo yote niliyokuambia.
3. Kwa maana, tazama, siku zinakuja, asema BWANA, nitakapowarejeza watu wangu wa Israeli na Yuda waliofungwa, asema BWANA; nami nitawarudisha hata nchi niliyowapa baba zao, nao wataimiliki.