Yer. 23:37-40 Swahili Union Version (SUV)

37. Nawe utamwambia nabii hivi, BWANA amekujibu nini? Na, BWANA amesemaje?

38. Lakini mkisema, Mzigo wa BWANA, basi, BWANA asema hivi, Kwa sababu mwasema neno hili, “Mzigo wa BWANA”; nami nimemtuma mtu kwenu kusema, Msiseme, “Mzigo wa BWANA”;

39. basi, kwa hiyo angalieni, nitawasahau ninyi kabisa, nami nitawatupilia mbali, pamoja na mji huu niliowapa ninyi na baba zenu, mtoke mbele za uso wangu;

40. nami nitaleta juu yenu aibu ya milele, na fedheha ya daima, ambayo haitasahauliwa.

Yer. 23