1. Neno la BWANA likanijia, kusema,
2. Enenda ukalie masikioni mwa Yerusalemu, ukisema, BWANA asema hivi,Nakukumbuka, hisani ya ujana wako,upendo wa wakati wa uposo wako;Jinsi ulivyonifuata huko jangwani,katika nchi isiyopandwa mbegu.
3. Israeli walikuwa utakatifu kwa BWANA;malimbuko ya uzao wake;Wote watakaomla watakuwa na hatia;uovu utawajilia; asema BWANA.