1. Laiti ungekuwa kama ndugu yangu,Aliyeyanyonya matiti ya mamangu!Kama ningekukuta huko nje,Ningekubusu, asinidharau mtu.
2. Ningekuongoza nyumbani mwa mamangu,Naye angenifundisha;Ningekunywesha divai iliyokolea,Divai mpya ya mkomamanga wangu.
3. Mkono wake wa kushoto ungekuwa chini ya kichwa changu,Nao wa kuume ungenikumbatia.