1. Usiku kitandani nalimtafuta mpendwa wa nafsi yangu,Nalimtafuta, nisimpate.
2. Nikasema, Haya, niondoke nizunguke mjini,Katika njia zake na viwanjani,Nimtafute mpendwa wa nafsi yangu.Nikamtafuta, nisimpate.
3. Walinzi wazungukao mjini waliniona;Je! Mmemwona mpendwa wa nafsi yangu?
4. Kitambo kidogo tu nikiisha kuwaondokea,Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu;Nikamshika, nisimwache tena,Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu,Chumbani mwake aliyenizaa.
5. Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu,Kwa paa na kwa ayala wa porini,Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha,Hata yatakapoona vema yenyewe.