5. Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri,Enyi binti za Yerusalemu,Mfano wa hema za Kedari,Kama mapazia yake Sulemani.
6. Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi,Kwa sababu jua limeniunguza.Wana wa mamangu walinikasirikia,Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu;Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda.
7. Nijulishe, ee mpendwa wa nafsi yangu,Ni wapi utakapolisha kundi lako,Ni wapi utakapolilaza adhuhuri.Kwa nini niwe kama aliyefungiwa kidoto,Karibu na makundi ya wenzako?