Wim. 1:5-7 Swahili Union Version (SUV)

5. Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri,Enyi binti za Yerusalemu,Mfano wa hema za Kedari,Kama mapazia yake Sulemani.

6. Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi,Kwa sababu jua limeniunguza.Wana wa mamangu walinikasirikia,Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu;Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda.

7. Nijulishe, ee mpendwa wa nafsi yangu,Ni wapi utakapolisha kundi lako,Ni wapi utakapolilaza adhuhuri.Kwa nini niwe kama aliyefungiwa kidoto,Karibu na makundi ya wenzako?

Wim. 1