Ufu. 7:8-10 Swahili Union Version (SUV)

8. Wa kabila ya Zabuloni kumi na mbili elfu.Wa kabila ya Yusufu kumi na mbili elfu.Wa kabila ya Benyamini kumi na mbili elfu waliotiwa muhuri.

9. Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao;

10. wakilia kwa sauti kuu wakisema, Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.

Ufu. 7