Tit. 2:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima;

2. ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika saburi.

3. Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema;

4. ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

Tit. 2