Rut. 4:16-21 Swahili Union Version (SUV)

16. Basi Naomi akamtwaa yule mtoto, akamweka kifuani pake, akawa mlezi wake.

17. Nao wale wanawake waliokuwa jirani zake wakampa jina, wakisema, Naomi amezaliwa mwana; wakamwita jina lake Obedi; yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.

18. Hivi ndivyo vizazi vya Peresi; Peresi alimzaa Hesroni;

19. na Hesroni akamzaa Ramu; na Ramu akamzaa Aminadabu;

20. na Aminadabu akamzaa Nashoni; na Nashoni akamzaa Salmoni;

21. na Salmoni akamzaa Boazi; na Boazi akamzaa Obedi;

Rut. 4