Rut. 1:11-18 Swahili Union Version (SUV)

11. Naye Naomi akasema, Enyi wanangu, mrejee; kwani kufuatana na mimi? Je! Mimi ninao watoto wa kiume tena tumboni mwangu, hata wawe waume zenu?

12. Enyi wanangu, mrejee; nendeni zenu; kwa kuwa mimi ni mzee, siwezi kupata mume tena. Kama ningesema, Natumaini; kama ningepata mume hata usiku huu, na kuzaa watoto wa kiume;

13. je! Mngesubiri hata watakapokuwa watu wazima? Mngejizuia msiwe na waume? La, sivyo, wanangu; maana ni vigumu kwangu kuliko kwenu, kwa sababu mkono wa BWANA umetoka juu yangu.

14. Nao wakapaza sauti zao, wakalia tena, na Orpa akambusu mkwewe, lakini Ruthu akaambatana naye.

15. Naye akasema, Tazama, shemeji yako amerejea kwa watu wake, na kwa mungu wake; basi urejee wewe umfuate shemeji yako.

16. Naye Ruthu akasema,Usinisihi nikuache,Nirejee nisifuatane nawe;Maana wewe uendako nitakwenda,Na wewe ukaapo nitakaa.Watu wako watakuwa watu wangu,Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu;

17. Pale utakapokufa nitakufa nami,Na papo hapo nitazikwa;BWANA anitende vivyo na kuzidi,Ila kufa tu kutatutenga wewe nami.

18. Basi alipomwona kuwa amekaza nia yake kufuatana naye, aliacha kusema naye.

Rut. 1