28. Kwa maana Bwana atalitekeleza neno lake juu ya nchi, akilimaliza na kulikata.
29. Tena kama Isaya alivyotangulia kunena,Kama Bwana wa majeshi asingalituachia uzao,Tungalikuwa kama Sodoma, tungalifananishwa na Gomora.
30. Tuseme nini, basi? Ya kwamba watu wa Mataifa, wasioifuata haki, walipata haki; lakini ni ile haki iliyo ya imani;
31. bali Israeli wakiifuata sheria ya haki hawakuifikilia ile sheria.