Rum. 9:22-26 Swahili Union Version (SUV)

22. Ni nini basi, ikiwa Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake, na kuudhihirisha uweza wake, kwa uvumilivu mwingi, alichukuliana na vile vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa tayari kwa uharibifu;

23. tena, ili audhihirishe wingi wa utukufu wake katika vile vyombo vya rehema, alivyovitengeneza tangu zamani vipate utukufu;

24. ndio sisi aliotuita, si watu wa Wayahudi tu, ila na watu wa Mataifa pia?

25. Ni kama vile alivyosema katika Hosea,Nitawaita watu wangu wale wasiokuwa watu wangu,Na mpenzi wangu yeye asiyekuwa mpenzi wangu.

26. Tena itakuwa mahali pale walipoambiwa,Ninyi si watu wangu,Hapo wataitwa wana wa Mungu aliye hai.

Rum. 9