1. Kwa hiyo, wewe mtu uwaye yote uhukumuye, huna udhuru; kwa maana katika hayo umhukumuyo mwingine wajihukumu mwenyewe kuwa na hatia; kwa maana wewe uhukumuye unafanya yale yale.
2. Nasi twajua ya kuwa hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao hayo.