19. kwa nguvu za ishara na maajabu, katika nguvu za Roho Mtakatifu; hata ikawa tangu Yerusalemu, na kando kando yake, mpaka Iliriko nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa utimilifu;
20. kadhalika nikijitahidi kuihubiri Injili, nisihubiri hapo ambapo jina la Kristo limekwisha kutajwa, nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine;
21. bali kama ilivyoandikwa,Wale wasiohubiriwa habari zake wataona,Na wale wasiojasikia watafahamu.
22. Ndiyo sababu nalizuiwa mara nyingi nisije kwenu.