Rum. 15:19-22 Swahili Union Version (SUV)

19. kwa nguvu za ishara na maajabu, katika nguvu za Roho Mtakatifu; hata ikawa tangu Yerusalemu, na kando kando yake, mpaka Iliriko nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa utimilifu;

20. kadhalika nikijitahidi kuihubiri Injili, nisihubiri hapo ambapo jina la Kristo limekwisha kutajwa, nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine;

21. bali kama ilivyoandikwa,Wale wasiohubiriwa habari zake wataona,Na wale wasiojasikia watafahamu.

22. Ndiyo sababu nalizuiwa mara nyingi nisije kwenu.

Rum. 15