Rum. 12:18-21 Swahili Union Version (SUV)

18. Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.

19. Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.

20. Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake.

21. Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

Rum. 12