Rum. 12:17-20 Swahili Union Version (SUV)

17. Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.

18. Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.

19. Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.

20. Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake.

Rum. 12