25. Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
26. Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa,Mwokozi atakuja kutoka Sayuni;Atamtenga Yakobo na maasia yake.
27. Na hili ndilo agano langu nao,Nitakapowaondolea dhambi zao.
28. Basi kwa habari ya Injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu.
29. Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake.