Rum. 10:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.

2. Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa.

3. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.

4. Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.

Rum. 10