13. Ni kwa sababu ya dhambi za manabii wakeNa maovu ya makuhani wake,Walioimwaga damu ya wenye hakiKatikati yake.
14. Hutanga-tanga njiani kama vipofu,Wametiwa unajisi kwa damu;Hata ikawa watu wasiwezeKuyagusa mavazi yao.
15. Watu waliwapigia kelele, Ondokeni, Uchafu,Ondokeni, ondokeni, msiguse;Walipokimbia na kutanga-tanga, watu walisema kati ya mataifa,Hawatakaa hapa tena.
16. Hasira ya BWANA imewatenga,Yeye hatawaangalia tena;Hawakujali nafsi za wale makuhani,Hawakuwaheshimu wazee wao.
17. Macho yetu yamechokaKwa kuutazamia bure msaada wetu;Katika kungoja kwetu tumengojea taifaLisiloweza kutuokoa.
18. Wanatuvizia hatua zetu,Hata hatuwezi kwenda katika njia zetu;Mwisho wetu umekaribia, siku zetu zimetimia;Maana mwisho wetu umefika.
19. Waliotufuatia ni wepesiKuliko tai za mbinguni;Hao walitufuatia milimani,Nao walituotea jangwani.
20. Pumzi ya mianzi ya pua zetu, masihi wa BWANA,Alikamatwa katika marima yao;Ambaye kwa habari zake tulisema,Chini ya kivuli chake tutakaa kati ya mataifa.
21. Furahi, ushangilie, Ee binti Edomu,Ukaaye katika nchi ya Usi;Hata kwako kikombe kitapita,Utalewa, na kujifanya uchi.
22. Uovu wako umetimia, Ee binti Sayuni;Hatakuhamisha tena;Atapatiliza uovu wako, Ee binti Edomu;Atazivumbua dhambi zako.