1. Jinsi dhahabu ilivyoacha kung’aa,Na dhahabu iliyo safi ilivyobadilika!Mawe ya patakatifu yametupwaMwanzo wa kila njia.
2. Wana wa Sayuni wenye thamani,Walinganao na dhahabu safi,Jinsi wanavyodhaniwa kuwa vyombo vya udongo,Kazi ya mikono ya mfinyanzi!