Omb. 3:8-20 Swahili Union Version (SUV)

8. Naam, nikilia na kuomba msaada,Huyapinga maombi yangu.

9. Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa;Ameyapotosha mapito yangu.

10. Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye,Kama simba aliye mafichoni.

11. Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua;Amenifanya ukiwa.

12. Ameupinda upinde wake,Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.

13. Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.

14. Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.

15. Amenijaza uchungu,Amenikinaisha kwa pakanga.

16. Amenivunja meno kwa changarawe;Amenifunika majivu.

17. Umeniweka nafsi yangu mbali na amani;Nikasahau kufanikiwa.

18. Nikasema, Nguvu zangu zimepotea,Na tumaini langu kwa BWANA.

19. Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu,Pakanga na nyongo.

20. Nafsi yangu ikali ikiyakumbuka hayo,Nayo imeinama ndani yangu.

Omb. 3