7. Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka;Ameufanya mnyororo wangu mzito.
8. Naam, nikilia na kuomba msaada,Huyapinga maombi yangu.
9. Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa;Ameyapotosha mapito yangu.
10. Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye,Kama simba aliye mafichoni.
11. Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua;Amenifanya ukiwa.
12. Ameupinda upinde wake,Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.
13. Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.