Omb. 3:6-15 Swahili Union Version (SUV)

6. Amenikalisha penye giza,Kama watu waliokufa zamani.

7. Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka;Ameufanya mnyororo wangu mzito.

8. Naam, nikilia na kuomba msaada,Huyapinga maombi yangu.

9. Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa;Ameyapotosha mapito yangu.

10. Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye,Kama simba aliye mafichoni.

11. Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua;Amenifanya ukiwa.

12. Ameupinda upinde wake,Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.

13. Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.

14. Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.

15. Amenijaza uchungu,Amenikinaisha kwa pakanga.

Omb. 3