58. Ee BWANA umenitetea mateto ya nafsi yangu;Umeukomboa uhai wangu.
59. Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee BWANA;Unihukumie neno langu.
60. Umekiona kisasi chao chote,Na mashauri yao yote juu yangu.
61. Ee BWANA, umeyasikia matukano yao,Na mashauri yao yote juu yangu;
62. Midomo yao walioinuka juu yanguNa maazimio yao juu yangu mchana kutwa.
63. Uangalie kuketi kwao, na kuinuka kwao;Wimbo wao ndio mimi.
64. Utawalipa malipo, Ee BWANA,Sawasawa na kazi ya mikono yao.