Omb. 3:56-64 Swahili Union Version (SUV)

56. Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lakoIli usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu.

57. Ulinikaribia siku ile nilipokulilia;Ukasema, Usiogope.

58. Ee BWANA umenitetea mateto ya nafsi yangu;Umeukomboa uhai wangu.

59. Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee BWANA;Unihukumie neno langu.

60. Umekiona kisasi chao chote,Na mashauri yao yote juu yangu.

61. Ee BWANA, umeyasikia matukano yao,Na mashauri yao yote juu yangu;

62. Midomo yao walioinuka juu yanguNa maazimio yao juu yangu mchana kutwa.

63. Uangalie kuketi kwao, na kuinuka kwao;Wimbo wao ndio mimi.

64. Utawalipa malipo, Ee BWANA,Sawasawa na kazi ya mikono yao.

Omb. 3