44. Umejifunika nafsi yako kwa wingu,Maombi yetu yasipite.
45. Umetufanya kuwa takataka, na vifusiKatikati ya mataifa.
46. Juu yetu adui zetu woteWametupanulia vinywa vyao.
47. Hofu imetujilia na shimo,Ukiwa na uharibifu.
48. Jicho langu lachuruzika mito ya majiKwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu.
49. Jicho langu latoka machozi lisikome,Wala haliachi;
50. Hata BWANA atakapoangaliaNa kutazama toka mbinguni.
51. Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu,Kwa sababu ya binti zote za mji wangu.
52. Walio adui zangu bila sababuWameniwinda sana kama ndege;
53. Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani,Na kutupa jiwe juu yangu.
54. Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu,Nikasema, Nimekatiliwa mbali.
55. Naliliitia jina lako, BWANA, kutoka lile shimoLiendalo chini kabisa.
56. Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lakoIli usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu.