Omb. 3:4-11 Swahili Union Version (SUV)

4. Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu;Ameivunja mifupa yangu.

5. Amejenga boma juu yangu,Na kunizungusha uchungu na uchovu.

6. Amenikalisha penye giza,Kama watu waliokufa zamani.

7. Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka;Ameufanya mnyororo wangu mzito.

8. Naam, nikilia na kuomba msaada,Huyapinga maombi yangu.

9. Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa;Ameyapotosha mapito yangu.

10. Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye,Kama simba aliye mafichoni.

11. Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua;Amenifanya ukiwa.

Omb. 3