4. Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu;Ameivunja mifupa yangu.
5. Amejenga boma juu yangu,Na kunizungusha uchungu na uchovu.
6. Amenikalisha penye giza,Kama watu waliokufa zamani.
7. Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka;Ameufanya mnyororo wangu mzito.
8. Naam, nikilia na kuomba msaada,Huyapinga maombi yangu.
9. Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa;Ameyapotosha mapito yangu.
10. Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye,Kama simba aliye mafichoni.
11. Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua;Amenifanya ukiwa.