Omb. 3:38-43 Swahili Union Version (SUV)

38. Je! Katika kinywa chake Aliye juuHayatoki maovu na mema?

39. Mbona anung’unika mwanadamu aliye haiMtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?

40. Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu,Na kumrudia BWANA tena.

41. Na tumwinulie Mungu aliye mbinguniMioyo yetu na mikono.

42. Sisi tumekosa na kuasi;Wewe hukusamehe.

43. Umetufunika kwa hasira na kutufuatia;Umeua, wala hukuona huruma.

Omb. 3