Omb. 3:12-19 Swahili Union Version (SUV)

12. Ameupinda upinde wake,Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.

13. Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.

14. Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.

15. Amenijaza uchungu,Amenikinaisha kwa pakanga.

16. Amenivunja meno kwa changarawe;Amenifunika majivu.

17. Umeniweka nafsi yangu mbali na amani;Nikasahau kufanikiwa.

18. Nikasema, Nguvu zangu zimepotea,Na tumaini langu kwa BWANA.

19. Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu,Pakanga na nyongo.

Omb. 3