12. Ameupinda upinde wake,Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.
13. Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.
14. Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.
15. Amenijaza uchungu,Amenikinaisha kwa pakanga.
16. Amenivunja meno kwa changarawe;Amenifunika majivu.
17. Umeniweka nafsi yangu mbali na amani;Nikasahau kufanikiwa.
18. Nikasema, Nguvu zangu zimepotea,Na tumaini langu kwa BWANA.
19. Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu,Pakanga na nyongo.