Omb. 3:11-17 Swahili Union Version (SUV)

11. Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua;Amenifanya ukiwa.

12. Ameupinda upinde wake,Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.

13. Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.

14. Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.

15. Amenijaza uchungu,Amenikinaisha kwa pakanga.

16. Amenivunja meno kwa changarawe;Amenifunika majivu.

17. Umeniweka nafsi yangu mbali na amani;Nikasahau kufanikiwa.

Omb. 3